Marais wa nchi tano za Afrika na wakuu wa serikali wamehudhuria mkutano wa Kilele wa kujadili ubora wa udongo na mbolea barani Afrika, wakitoa wito wa uwepo wa mkakati wa pamoja, hatua za pamoja na uwekezaji ili kuiwezesha Afrika kuzalisha chakula cha kutosha.
Mahakama ya kijeshi katika mji wa Goma huko Kivu Kaskazini Mashariki mwa Congo imewahukumu kifo maafisa nane wa jeshi la Congo, FARDC kwa tuhuma za kukimbia vita na kutoheshimu sheria za kijeshi.
Mwaka huu Sherehe za Siku ya Kimataifa ya Wafanyakazi zina hisia ya dharura ya kujitolea upya kwa haki za kijamii, wakati tunapopitia kipindi kigumu, ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa na mabadiliko ya haraka katika sehemu za kazi kutokana na maendeleo ya teknolojia.
Mafuriko makubwa yameyakumba maeneo mengi ya Afrika Mashariki ambayo yanakabiliwa na mvua za mfululizo, Burundi ikiomba msaada wa kimataifa wa kuisaidia kupambana na maafa hayo.
Wakulima nchini Kenya waliopewa mbolea ghushi watafidiwa na serikali ya Kenya baada ya kampuni moja kutajwa kuwahadaa wakulima na hivyo kuiweka serikali katika hali ngumu kufuatia Sakata hilo.
Gavana wa Jimbo la Maryland, Wes Moore, ameweka wazi kuwa hapakuwa na kitendo chochote cha kigaidi baada ya daraja kuu katika mji wa Baltimore kubomoka Jumanne asubuhi wakati meli iliyobeba mizigo kugonga nguzo yake.
Wawakilishi wa Burundi katika michuano ya mwaka huu ya Ligi ya Mpira wa Kikapu Afrika- BAL katika mashindano yanayofadhiliwa na Chama cha mpira wa Kikapu NBA tawi la Afrika Jumatatu walipoteza ushiriki wao baada ya kukataa kuvaa jezi yenye nembo ya Visit Rwanda.
Mungano wa asasi za kiraia nchini Senegal umetangaza kuundwa kwa mungano mpya na vyama vya kisiasa ili kutayarisha uchaguzi wa rais kabla ya tarehe 2 mwezi Aprili.
Rais wa zamani wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi, amefariki leo Alhamisi akiwa na umri wa miaka 98, vyanzo vya habari nchini Tanzania vimeeleza.
Mwili wa raia wa Tanzania umepatikana ukielea katika Mto Miami Marekani Jumanne asubuhi na idara husika zikithibitisha kuwa mwili huo ni wa mtu aliyeanguka kutoka katika mashua mwishoni mwa juma.
Wahifadhi wa mazingira na wanyama pori wa Afrika Kusini wameonya Jumanne kwamba kuna ongezeko kubwa la ujangili wa wanyama pori, wakiwemo wanyama takriban 500 wameuawa mwaka jana.
Baadhi ya wachumi na wasomi nchini Tanzania weitaka serikali kuhakikisha mradi wa reli ya umeme SGR unaleta manufaa kwa wananchi wa matabaka yote kwa kutoa huduma zenye bei nafuu huku wakishauri mradi huo ujikite katika usafirishaji wa mizigo ili kuhakikisha unarudisha uwekezaji uliofanyika.
Kauli mbiu ya Siku ya Radio Duniani mwaka 2024 inaangazia kwa upana mafanikio ya radio yaliyofikiwa siku za nyuma, uhalisia wake hivi sasa na maendeleo ya mustakbali wake.
Kukosekana kwa uhuru wa vyombo vya habari kutoa baadhi ya habari pamoja na kuwepo kwa idadi kubwa ya kodi na tozo ni miongoni mwa changamoto zinazosababisha ugumu katika uendeshaji wa vyombo vya habari nchini Tanzania .