Kennes Bwire is a journalist with Voice of America and is based in Washington DC.
Ndege za kijeshi za jamhuri ya kidemokrasia ya Congo zimeendelea kushambulia waasi wa kundi la M23 wanaoshikilia mji wa Kitchanga, Kivu kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imeonya kwamba haitaendelea kuvumilia kile imekitaja kama unyanyasaji wa jirani yake Rwanda, licha ya kutakiwa kufuata utaratibu wa kuleta amani mashariki mwa nchi hiyo na kwamba ina haki ya kujilinda na kulinda ardhi yake kwa nguvu zote.
Serikali ya Rwanda imesema kwamba Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC inasajili mamluki na kuvuruga mchakato wa kuleta amani nchini humo.
Rais wa Rwanda Paul Kagame amesema kwamba kundi la waasi la Democratic Forces for Liberation of Rwanda - FDLR, linaloshutumiwa na serikali ya Rwanda kwa kusababisha mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 linaungwa mkono na baadhi ya watu kwa lengo la kuipindua serikali yake.
Mawaziri nchini Uganda wameendelea kumkosoa mtoto wa rais Yoweri Museveni baada ya kuonyesha dalili za kutaka kugombea urais na badala yake wameanza kampeni ya kuhakikisha kwamba Museveni anagombea mhula mwingine madatakani katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2026.
Majenerali waliosaidia rais wa Uganda Yoweri Museveni kuingia madarakani, wanaendelea kutoa hisia zao hadharani kuhusiana na tabia ya mtoto wa Museveni Generali Muhoozi Kainerugaba kuwakosoa, kukosoa chama chao cha NRM na kujihusisha na siasa.
Serikali ya Marekani imeambia Rwanda kuondoa wanajeshi wake kutoka sehemu za Kivu kaskazini, mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, ambapo serikali ya rais Paul Kagame inaripotiwa kuwasaidia waasi wa kundi la M23.
Wawakilishi wa chama cha Republican hawajaelewena kuhusu mmoja wao wanayestahili kumuunga mkono na kumchagua kuwa spika wa baraza la wawakilishi.
Shirika la amnesty international linataka serikali ya Tanzania kufuta sheria zote zilizoundwa kutokana na kile imetaja kama amri ya rais na ambazo raia wa Tanzania wanaziona kama sheria kandamizi.
Uhusiano kati ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na Jirani yake Rwanda, umeendelea kuwa mbaya, baada ya serikali ya DRC kutangaza kuwakamata watu wanne kwa madai kwamba walikuwa wanapanga kuangusha ndege ya rais Felix Tshisekedi.
Ripoti ya umoja wa mataifa kuhusu vita vya waasi mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo inawatuhumu waasi wa kundi la M23 kwa mauaji ya Watoto na akina mama, kuwateka watu nyara, unajisi na mateso mengine ya raia.
Matukio mengi Afrika mwaka 2022 yamezunguka sana Afrika magharibi kutokana na ukosefu wa usalama na mapinduzi ya kijeshi.
Tume maalum iliyoundwa kuchunguza makamishna 4 wa tume huru ya uchaguzi nchini Kenya IEBC, imeambiwa kwamba makamishna hao walikuwa wanashirikiana na maafisa wa ngazi ya juu serikalini, na mkurugenzi mkuu wa muungano wa Azimio wa Raila Odinga, Raphael Tuju kulazimisha duru ya pili ya uchaguzi mkuu.
Cyril Ramaphosa, rais wa Afrika kusini, amechaguliwa wiki hii kuwa mwenyekiti wa chama kinachotawala cha African national Congress ANC.
Serikali ya Tanzania imetangaza kupokea mkopo wa dola bilioni 2.2 kutoka China ili kusaidia kukamilisha ujenzi wa reli ya mwendo wa wastani SGR.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kwamba haoni makosa yoyote kwa mwanawe kuzungumzia siasa za nchi hiyo licha ya kwamba sheria za nchi zinapiga marufuku wanajeshi kuzungumzia au kujihusisha na siasa.
Mfanyabiashara maarufu, mwanasiasa na aliyekuwa gavana wa mkoa wa Katanga, Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo Moise Katumbi, ametangaza kwamba atagombea urais katika uchaguzi mkuu wa Desemba mwaka ujao 2023.
Mwanajeshi wa Uganda ameuawa katika mapambano na waasi wa kundi la Allied Democratic Forces ADF waliovuka mpaka kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuingia katika wilaya ya Ntoroko, magharibi mwa Uganda.
Deni la serikali ya Tanzania linaendelea kuongezeka kila mwezi kwa kiasi cha dola milioni 544.8. Haya ni kulingana na ripoti ya benki kuu ya nchi hiyo - BoT.
Rais wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi amesema kwamba atafanya kila awezalo kuhakikisha kwamba jeshi la nchi hiyo lina nguvu na uwezo wa kulinda nchi dhidi ya kila aina ya adui.
Pandisha zaidi