Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Mei 12, 2024 Local time: 08:37

Washukiwa wanamgambo wa Kiislam wateka nyara watu 50 wiki hii Nigeria


Rais wa Nigeria Bola Tinubu akiwa Ikulu huko Abuja Januari 23, 2024. Picha na ANDREW CABALLERO-REYNOLDS / POOL / AFP.
Rais wa Nigeria Bola Tinubu akiwa Ikulu huko Abuja Januari 23, 2024. Picha na ANDREW CABALLERO-REYNOLDS / POOL / AFP.

Watu wanaoshukiwa kuwa waasi wa Kiislamu waliwateka nyara watu 50, wengi wao wakiwa wanawake, kaskazini mashariki mwa Nigeria wiki hii, maafisa wa eneo hilo na mkazi mmoja walisema Jumatano, utekaji nyara wa hivi karibuni zaidi wa wapiganaji ambao wameendesha uasi kwa zaidi ya muongo mmoja.

Watu wanaoshukiwa kuwa waasi wa Kiislamu waliwateka nyara watu 50, wengi wao wakiwa wanawake, kaskazini mashariki mwa Nigeria wiki hii, maafisa wa eneo hilo na mkazi mmoja walisema Jumatano, utekaji nyara wa hivi karibuni zaidi wa wapiganaji ambao wameendesha uasi kwa zaidi ya muongo mmoja.

Wapiganaji wa Boko Haram na wa Islamic West Africa Province (ISWAP) wamekuwa wakiendesha shughuli zao katika jimbo la Borno kaskazini mashariki, wakilenga vikosi vya usalama na raia, katika harakati hiyo ya kuua na kuwafukuza maelfu ya watu.

Tukio la hivi karibuni lilitokea Jumatatu katika eneo la mbali la Gamboru, ambalo linapakana na Chad na Cameroon, alisema afisa wa Kikosi Kazi cha Pamoja cha Wananchi, ambacho husaidia jeshi kupambana na wanajihadi.

Afisa huyo ambaye alikataa kutaja jina lake kwa sababu hana kibali cha kuzungumza na vyombo vya habari, alisema kundi hilo la watu wasiopungua 50 kutoka kambi ya wakimbizi wa ndani, walikwenda kukusanya kuni katika mwambao wa Ziwa Chad, ambako ISWAP inajulikana. kufanya operesheni zake.

Forum

XS
SM
MD
LG