Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 03, 2024 Local time: 20:03

Viongozi wa Afrika wazungumzia athari za Mabadiliko ya Hali ya Hewa Afrika kabla ya COP28

Rais wa Kenya William Ruto, Jumatatu, amefungua mkutano wa kilele wa hali ya hewa barani Afrika na kuwaomba wajumbe waliohudhuria kutumia mkutano huo kusaidia kutoa mapendekezo ya Afrika kwenye mkutano ujao wa hali ya hewa wa COP28 utakaofanyika Dubai mwezi Novemba.

Ruto amewaeleza wajumbe wanaojumuisha wakuu wa nchi, watunga sera, viongozi wa serikali, watoa maamuzi, wataalam wa mabadiliko ya tabianchi, mashirika ya kimataifa na mashirika ya kiraia, na sekta binafsi kuwa wakati umefika sasa wa bara la Afrika kutafuta ufumbuzi wa kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa barani Afrika.

Ruto, kando na kuwataka viongozi wa Kiafrika na kimataifa, wafuatiliaji wa uvumbuzi, wataalam, wawekezaji, na wakuu wa tasnia mbalimbali kulitumia jukwaa hili kama ukumbi wa majadiliano kuchunguza mawazo, kutathmini mitazamo, na kufungua masuluhisho kwa siku tatu zijazo, amewarai wajumbe kubuni mkakati wa kubadilisha utajiri wa rasilimali za Afrika kutoka kwa uwezo hadi kuwa fursa halisi, kwa kuelekeza uwekezaji mkubwa ambao utafanikisha uwezekano uliopo kuvinufaisha vizazi vya sasa na vijavyo.


Pandisha zaidi

Makundi

XS
SM
MD
LG