Vyanzo kadhaa vya habari wakiwemo wakaazi wa sehemu hiyo na maafisa wa afya wamethibitisha tukio hilo.
Wamesema kwamba kilipuzi kilichokuwa kimetegwa kwenye pikipiki kililipuka wakati msafara wa Taliban ulipokuwa unapita katika mji wa Faizabad.
Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani Abdul Mateen Qani amethibitisha tukio hilo na kusema kwamba bomu hilo lilikuwa limewalenga maafisa wa usalama waliokuwa wanaelekea katika shughuli za kuharibu mabomu.
Qatani amesema uchunguzi unaendelea.
Hakuna kundi kufikia sasa limedai kuhusika katika sehemu hiyo ya Badakhshan ambapo kumekuwa na maandamano mabaya ya raia dhidi ya utawala wa Taliban.
Maandamano ya ijumaa yalisababisha vifo vya waandamanaji wawili baada ya kutokea makabiliano na maafisa wa usalama.
Forum