Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 03, 2024 Local time: 22:57

Rais wa Iran anaitembelea Pakistan siku ya Jumatatu


Rais wa Iran, Ebrahim Raisi. March 20, 2024. (Iranian Presidency Office via AP)
Rais wa Iran, Ebrahim Raisi. March 20, 2024. (Iranian Presidency Office via AP)

Tangazo kutoka wizara ya mambo ya nje ya Islamabad lilisema ziara hii itatoa fursa muhimu kuimarisha uhusiano wa nchi mbili

Rais wa Iran Ebrahim Raisi atawasili katika nchi jirani ya Pakistan Jumatatu kwa ajili ya mikutano rasmi na viongozi wa taifa hilo huku kukiwa na mivutano kati ya Iran na Israel.

Tangazo kutoka wizara ya mambo ya nje ya Islamabad leo Jumapili lilisema kuwa mazungumzo hayo yatatoa fursa muhimu ya kuimarisha uhusiano wa nchi mbili na ushirikiano katika biashara, mawasiliano, nishati, na kilimo.

Tangazo lilisema ujumbe wa ngazi ya juu wa Raisi utawajumuisha waziri wa mambo ya nje wa Iran, mawaziri wengine na wawakilishi wa biashara. Wakati wa ziara yake ya siku tatu nchini Pakistan, rais wa Iran anatarajiwa kukutana na mwenzake, Asif Ali Zardari, na Waziri Mkuu Shehbaz Sharif, miongoni mwa wengine.

Taarifa ya Pakistan imesema bila kufafanua, pia watajadili maendeleo ya kikanda na kimataifa na ushirikiano wa nchi hizi mbili ili kupambana na tishio la pamoja la ugaidi.

Forum

XS
SM
MD
LG