Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Mei 20, 2024 Local time: 03:02

Japan inavutana na Russia kuhusu umiliki wa kisiwa


Silaha iliyozeeka kwenye kisiwa cha Kunashiri kinachozozaniwa na Japan na Russia
Silaha iliyozeeka kwenye kisiwa cha Kunashiri kinachozozaniwa na Japan na Russia

Mivutano kati ya Japan na Russia itaendelea kuongezeka kutokana na vita huko nchini Ukraine, huku kukiwa hakuna ishara za mgogoro wa ardhi wa muongo mzima kumalizika.

Kremlin ilipiga marufuku meli zisizo za Russia kuingia katika maji yaliyo karibu na visiwa vya Kuril – vinavyojulikana na Japan kama maeneo ya kaskazini – ambayo kwa sasa yanakaliwa na Russia lakini Japan inadai umiliki wake.

Tokyo inachukulia hatua hiyo kama sehemu ya vitisho kadhaa kutoka Moscow baada ya ushirikiano wa hivi karibuni kati ya Marekani na Japan.

Mapema mwaka huu, rais wa Russia Vladimir Putin alisema kwamba atavitembelea visiwa vya Kuril, hatua iliyopelekea kufifia kwa mazungumzo kuhusu umiliki wa visiwa hivyo vinavyozozaniwa na nchi hizo mbili.

Forum

XS
SM
MD
LG