Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 03, 2024 Local time: 22:43

Ghana yapiga hatua katika mpango wa misamaha ya madeni


Wabunge wa bunge la Ghana wakiwa bungeni huko Accra, Ghana Januari 7, 2021. Photo by Nipah Dennis / AFP.
Wabunge wa bunge la Ghana wakiwa bungeni huko Accra, Ghana Januari 7, 2021. Photo by Nipah Dennis / AFP.

Waziri wa Fedha wa Ghana anatarajia rasimu ya Mkataba wa Maelewano (MoU) kutoka kwa wakopeshaji wa nchi hiyo mwezi Mei kuhusu mpango wa marekebisho ya wakoeshaji Jumapili.

Makubaliano hayo, mara tu yatakapotiwa saini, yataimarisha mkataba wa kurekebisha mikopo ya dola bilioni 5.4 na wadai wake wakuu, zikiwemo China na Ufaransa, zilizokubaliwa mwezi Januari.

Marekebisho hayo ni hatua muhimu katika jitihada za Ghana za misamaha ya madeni huku ikipanga njia yake ya kutoka kwenye mgogoro mbaya zaidi wa kiuchumi katika muda mrefu na inapaswa kufungua sehemu zaidi za mpango wake wa dola bilioni 3 na IMF.

Akizungumza kandoni mwa mikutano ya IMF na Benki ya Dunia ya majira ya machipuko mjini Washington, Mohammed Amin Adam pia alisema ana imani bodi kuu ya Shirika la Fedha Duniani itaidhinisha mwezi Juni mapitio ya makubaliano yake ya ngazi ya wafanyakazi.

Forum

XS
SM
MD
LG