Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Mei 20, 2024 Local time: 08:15

Dola milioni 26 zachangiswa kwa ajili ya kampeni za Biden mjini New York


Rais wa zamani wa Marekani, Barack Obama, rais wa sasa Joe Biden, na Bill Clinton wakiwa New York Alhamisi usiku, kwenye hafla ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kampeni. Mei 28, 2024
Rais wa zamani wa Marekani, Barack Obama, rais wa sasa Joe Biden, na Bill Clinton wakiwa New York Alhamisi usiku, kwenye hafla ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kampeni. Mei 28, 2024

Barack Obama, Bill Clinton pamoja na watu wenye majina makubwa kwenye tasnia ya burudani waliungana pamoja  huko New York Alhamisi usiku kumkaribisha rais Joe Biden ambaye amechangisha kiwango kikubwa cha fedha dola milioni 26 kwa  kampeni yake ya kuchaguliwa.

Hali ilikuwa ya kusisimua kwenye ukumbi wa Radio City Music ambapo Obama alimsifu Biden kwa kuwa na msimamo wenye kuzingatia kila mmoja, akisema kuwa ,” Huyo ndiyo rais tunayemtaka.”

Clinton kwa upande wake alisema kwamba miongoni mwa wanaowania kwenye uchaguzi wa mwaka huu, “Ni bora kubaki na anayefanya kazi.” Biden kwa upande wake alimtaja mpinzani wake Donald Trump moja kwa moja, akisema kwamba mipango ya mgombea huyo wa chama cha Repablikan imepitwa na wakati na wala haifai.

Aliyeongoza hafla hiyo Stephen Colbert, wakati akizungumza na viongozi hao watatu aliwaita “ mabingwa wa kuzungumza,” akitania kuwa wote walifika New York, siyo kwa ajili ya kufika mahakamani, akizungumzia matatizo mengi ya kisheria yanayomkabili Trump.

Hafla hiyo ya uchangishaji fedha ilikuwa ni uungaji mkono mkubwa wa chama cha Demokratic kwa Biden, wakati ukusanyaji maoni ukionyesha uungaji mkono mdogo.

Forum

XS
SM
MD
LG