Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Mei 20, 2024 Local time: 15:33

Blinken asema hatua za Israel kuongeza mtiririko wa misaada Gaza zakaribishwa


Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wakikagua mabaki ya gari iliyokuwa ikitumiwa na Kikundi cha msaada cha World Central Kitchen chenye makao makuu Marekani, ambalo lilipigwa na kombora la Israeli huko Deir al-Balah, katikati ya Ukanda wa Gaza April 2, 2024.
Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wakikagua mabaki ya gari iliyokuwa ikitumiwa na Kikundi cha msaada cha World Central Kitchen chenye makao makuu Marekani, ambalo lilipigwa na kombora la Israeli huko Deir al-Balah, katikati ya Ukanda wa Gaza April 2, 2024.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken amesema hatua zilizotangazwa na serikali ya Israel kuongeza mtiririko wa misaada huko Gaza zinakaribishwa.

Hata hivyo Blinken amesema hatua hizo hazitoshi kukidhi matakwa ya utawala wa Rais Joe Biden kwa ajili ya kuboresha hali ya kibinadamu katika eneo hilo.

Waziri Blinken amefafanua Ijumaa kwamba mpaka pale hatua hizo zitakapo tekelezwa kikamilifu, kufunguliwa vivuko zaidi vya mpakani kunaweza kuongeza misaada kwa Wapalestina waliojikuta katika mapigano baina ya Israel na Hamas.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani ameeleza haya:

“ Haya ni maendeleo chanya, lakini mtihani wa kweli ni matokeo na ndiyo tunacho tazamia kuona katika siku za karibuni na wiki zijazo. Je misaada inawafikia watu wenye shida, kote Gaza?

Je ucheleweshwo mwingine kwenye vivuko vya mpakani umetatuliwa? Je tuna mfumo bora zaidi wa kutatua mgogoro na uratibu ili wafanyakazi wa misaada, wanaopeleka msaada wanaweza kufanya hivyo kwa hali salama na yenye uhakika? Mambo yote haya ni muhimu , na yana hitaji kupimwa na matokeo.”

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu

Ofisi ya waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ilitangaza Ijumaa kwamba Israel itachukua hatua kuboresha hali ikiwemo kufungua kivuko muhimu cha mpaka kuingia Gaza saa kadhaa baada ya rais wa Marekani Joe Biden kumwambia Alhamisi kwa njia ya simu kwamba msaada wa Marekani kwa ajili ya vita huko Gaza utategemea na Israel kuchukua hatua zaidi kuwalinda raia na wafanyakazi wa msaada.

Forum

XS
SM
MD
LG