Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Mei 19, 2024 Local time: 21:41

Benki kuu ya Kenya yapunguza makadirio yake ya ukuaji wa uchumi


Rais wa Kenya William Ruto akizungumza na waandishi wa habari katika Ikulu ya Nairobi, Terehe 2 Aprili 2023. Picha na Tony KARUMBA/AFP.
Rais wa Kenya William Ruto akizungumza na waandishi wa habari katika Ikulu ya Nairobi, Terehe 2 Aprili 2023. Picha na Tony KARUMBA/AFP.

Benki kuu ya Kenya imepunguza makadirio yake ya ukuaji wa uchumi kwa mwaka huu hadi asilimia 5.5, maelezo ya gavana wa benki hiyo Patrick Njoroge yalibainisha hivi leo Jumatano.

Benki kuu ya Kenya imepunguza makadirio yake ya ukuaji wa uchumi kwa mwaka huu hadi asilimia 5.5, maelezo ya gavana wa benki hiyo Patrick Njoroge yalibainisha hivi leo Jumatano.

Benki hiyo ilisema mwezi Machi kwamba uchumi ungepanuka kwa asilimia 5.8. Njoroge hakuelezea utabiri huo mpya. Uchumi ulipanuka kwa asilimia 4.8 mwaka jana,ikiwa ni chini ya kasi ya ukuaji wa mwaka 2021 uliolemewa na mdororo katika sekta ya kilimo.

Njoroge, ambaye atauacha wadhifa huo katikati ya mwezi ujao baada ya miaka minane, alisema alitarajia sekta ya kilimo itaimarika kutokana na athari za kudorora za mwaka jana na mvua za kutosha zimenyesha kote nchini.

Kilimo kinachangia pato kubwa la uchumi katika taifa hilo. Utalii, ni sekta nyingine muhimu inaripoti mustakabali mzuri wa siku zijazo gavana alisema, akiashiria utendaji mzuri katika miezi ijayo.

Forum

XS
SM
MD
LG