Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 11:40

Buhari azuru Cameroon.


Rais wa Cameroon Paul Biya na mwenzake wa Nigeria Muhammadu Buhari mjini Yaounde.
Rais wa Cameroon Paul Biya na mwenzake wa Nigeria Muhammadu Buhari mjini Yaounde.

Rais wa Nigeria jumatano amefanya ziara yake ya kwanza rasmi katika nchi jirani ya Cameroon wakati mataifa yote mawili yaliokuwa mahasimu yakishirikiana kukabiliana na tishio kutoka kwa kundi la Boko Haram ambalo limekuwa likitekeleza mashambulizi kwenye mataifa yote mawili.

Kiongozi huyo mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari ametembelea mji mkuu wa Cameroon kuunga mkono kikosi cha muungano kinachopambana na Boko Haram ambao wameuwa zaidi ya watu 60 katika siku za haivi karibuni nchini Cameroon.

​Ghasia kwenye eneo hilo zimewakosesha makao zaidi ya watu milioni 2 na kuuwa wengine 20,000 mahala ambapo mipaka ya Nigeria, Niger, Cameroon na Chad inapokutana katika kipindi cha miaka 6 iliopita tangu kundi hilo lilipojitokeza.

XS
SM
MD
LG