Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 02:07

Mwanasheria mkuu wa Tanzania kujiuzulu.


Rais J. Kikwete akimkabidhi miongozo ya kazi, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Tanzania, Jaji Frederick Werema huko Ikulu ya Tanzania.
Rais J. Kikwete akimkabidhi miongozo ya kazi, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Tanzania, Jaji Frederick Werema huko Ikulu ya Tanzania.

Mwanasheria mkuu wa Tanzania, Jaji Fredrick Werema, amejiuzulu Jumanne,Desemba16,2014.

Jaji Werema amewasilisha barua kwa Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete.

Katika taarifa rasmi iliyotolewa na ofisi ya Rais Ikulu, Jaji Werema amesema "ameomba kujiuzulu kwa sababu ushauri wake kuhusiana na suala la akaunti ya Tegeta Escrow, haukueleweka na umechafua hali ya hewa."

Akizungumza na Sauti ya Amerika mbunge wa Singida Mashariki ambaye pia ni mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu amesema ni hatua ambayo imechelewa sana. Hatua hii ilitakiwa kuchukuliwa muda mrefu uliopita.

please wait

No media source currently available

0:00 0:02:02 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Na ameongeza hatua hii haitoshi kutokana na ushahidi wa PAC kuna makosa makubwa ya jinai matumizi mabaya ya madaraka ufisadi na rushwa kwa hivyo hayawezi kuishia kwa kujiuzulu hii iwe ni hatua ya kwanza tu na kuna makosa ya jinai yanatakiwa yashughulikiwe.

XS
SM
MD
LG